Wapiganaji wa kundi la al-Shabab
walishambulia kambi ya jeshi nchini Somalia na kuidhibiti kwa muda
mapema asubuhi kusini magharibi mwa nchi hiyo.
Taarifa zinasema magari zaidi ya kumi ya jeshi la Somalia yaliuawa wakati wa shambulio hilo.
Msafara wa wanajeshi wa Somalia kutoka mji wa Baidoa, waliokuwa wakipelekwa kuwasaidia wenzao, pia ulishambuliwa.
Taarifa zinasema kulitokea vifo na majeruhi pande zote.
Mwandishi mmoja wa eneo hilo ameambia BBC kwamba wanajeshi 20 waliuawa wakati wa shambulio hilo.
Kikosi cha Umoja wa Afrika (Amisom) kimesema kupitia Twitter kwamba shambulio hilo lilitokea lakini kikakanusha taarifa kwamba kambi hiyo ilidhibitiwa na wapiganaji hao.
Kambi hiyo inapatikana kilomita 30 kutoka mji wa Baidoa.
Al-Shabab wamezidisha mashambulio dhidi ya wanajeshi wa Amisom na Somalia tangu katikati mwa mwaka jana.
Mapema mwaka huu, walishambulia kambi ya wanajeshi wa Kenya wanaohudumu chini ya Amisom.
Al-Shabab wamesema kwamba waliua zaidi ya wanajeshi 200 katika shambulio hilo eneo la El-Ade katika jimbo la Gedo tarehe 15 Januari mwaka huu.
Post a Comment