Latest in Tech

Kenya yailaumu Tanzania kuhusu raia wa Ethiopia

Ramani ya mpaka wa Kenya na Tanzania
Kenya imeilaumu Tanzania kwa kuwaweka raia wa Ethiopia katika eneo lake la mpaka siku ya Jumanne badala ya kuwarudisha makwao kulingana na ripoti ya gazeti la The standard nchini Kenya.

Raia hao wa Ethiopia walikuwa wamewachiliwa huru baada ya kuhudumia vifungo vya mashtaka tofauti ya uhalifu nchini Tanzania.

Maafisa wa polisi wameagizwa kutowaruhusu wageni hao kuingia nchini Kenya.

''Watarudishwa nchini Tanzania walikotoka.Kisa hicho hakikubaliki na hakiruhusiwi na sheria'',Afisa wa Kenya Henry Wafula alinukuliwa akisema.f

Share this:

Post a Comment

 
Copyright © bakinamimi. Designed by OddThemes & VineThemes