Wakuu wa jeshi wa Ukraine, wanasema kuwa ghasia zimezidi mashariki mwa nchi.
Wanasema
kuwa wapiganaqji wanaopendelea Urusi, wamevunja makubaliano ya
kusitisha mapigano, mara 30, katika saa 24 zilizopita, pamoja na
matumizi ya mizinga ambayo imepigwa marufuku katika mkataba wa Minsk. Inaarifiwa kuwa mabomba ya maji yaliyoharibika,
yamekata huduma kwa miji kama Luhansk, na wapiganaji wamekataa mabomba
hayo kutengenezwa.
Waziri wa Ulinzi wa Ukraine, Stepan Poltorak anasema Urusi inazidisha wanajeshi wake mpakani.
Post a Comment