![]() |
| James Clapper,mkuu wa upelelezi wa Marekani |
Mkurugenzi wa Upelelezi nchini
Marekani, James Clapper, amesema kuna ushahidi kwamba wavamizi wa
mitandao wanaofanya kazi na serikali za kigeni na wamejaribu kuwalenga
wagombea katika uchaguzi wa rais wa mwaka huu.
Lakini amesema anatarajia mashambulizi zaidi kwa jinsi kampeni zinavyoendelea.Maafisa hao wameitambua China kama chanzo cha mashambulizi dhidi ya wagombea wote wa Urais kutoka Democratic na Republican katika chaguzi mbili zilizopita.Mwaka huu makundi mbalimbali ya uvamizi mitandaoni yamekuwa yakitishia kampeni za bwana Donald Trump.


Post a Comment