Katika tamaduni nyingi kote duniani mwanamke anapoolewa huwa ni fahari kubwa sana akiwa ni bikira.
Mathalan ni dhihirisho la mwanamke kuwa amelelewa na kutunzwa vyema.
Ni dhihirisho la usafi.
Hata hivyo jamii moja nchini Malawi haithamini ubikira wa watoto wao wa kike.
Amini usiamini wazazi huwa wanamlipa ''Fisi'' kumbikiri binti yao punde tu anapopata hedhi yake ya kwanza.
Wanaamini kuwa binti ambaye ni bikira ni mkosi kwa jamii!
Malimwengu haya.
Wazazi na jamii kwa jumla katika maeneo mengi ya kusini mwa Malawi wamekuwa wakishikilia tamaduni hii kwa miaka na mikaka.
''Fisi'' ama wanaume wanaowabikiri watoto wa kike huchaguliwa na wazazi kuwaondolea mikosi.
Post a Comment