Latest in Tech

Waliofariki shambulio Baghdad wafika 250

Kundi la Islamic State limedai kuhusika
Wizara ya afya nchini Iraq inasema kuwa idadi ya watu ambao sasa wanajulikana kuuawa kwenye shambulizi la kujitolea mhanga siku ya Jumapili mjini Baghdad imeongezeka hadi watu 250.
Shambulizi hilo ambalo kundi la Islamic State lilidai kutekeleza, ndilo baya zaidi kuwai kutokea mjini Baghdad tangu Marekani iongoze uvamizi nchini Iraq mwaka 2003.
Ripoti ya Uingereza kuhusu uvamizi huo inatarajiwa kuchapishwa hii leo. Mwenyekiti wake anasema ana matumaini kuwa ripoti hiyo itahakikisha kuwa kuingilia kati kwa njia ya kijeshi kiwango kama hicho, hakuwezi kutokea siku za usoni bila ya kufanyika udadisi kwa njia ya uangalifu mkubwa.


Share this:

Post a Comment

 
Copyright © bakinamimi. Designed by OddThemes & VineThemes