Watu maarufu Tanzania wamekuwa wakizungukwa na mambo tofauti kwenye maisha yao haswa linapokuja swala la kutoa ushirikiano flani kwa vyama vya siasa,
Hivi karibuni kwenye mahojiano aliyofanyiwa Lulu ambaye ni mwigizaji mkubwa wa filamu na maigizo Tanzania aliulizwa Yeye shabiki wa chama gani cha siasa?
Elizabeth Michael ‘Lulu’ alijibu hivi “Mimi sina chama, ndiyo maana hata katika kampeni za Uchaguzi Mkuu mwaka jana, sijaonekana kwenye jukwaa lolote. Miye naamini kura ni siri na nilifanya hivyo ili nisifungamane na upande wowote.”
Lulu yupo kwenye ziara ya vyombo vya habari akitangaza filamu yake mpya ya NI NOMA.
Jacqueline Wolper, muigizaji aliyejipatia umaarufu mwaka jana kwa kuwa bega kwa bega na aliyekuwa mgombea urais kupitia tiketi ya Ukawa, Edward Lowassa, amejiunga rasmi na Chama cha Mapinduzi, CCM.
Wolper alitangaza kujiunga na chama hicho tawala Jumamosi iliyopita kwenye mkutano mkuu uliofanyika Dodoma ambapo pia Rais Dkt John Magufuli alichaguliwa kuwa mwenyekiti mpya.
Muigizaji huyo alishare kwenye Instagram picha ikimuonesha akimpa mkono Rais mstaafu, Dkt Jakaya Kikwete kwenye mkutano huo.
Picha hiyo hata hivyo imesababisha hasira nyingi kwa mashabiki wake ambao ni wapenzi wa upinzani huku wakimfananisha na Yuda Iskarioti kwa madai kuwa amewasaliti Ukawa.
Mgombea urais wa chama cha Republican nchini Marekani Donald Trump amemsifu kiongozi wa zamani wa Iraq Saddam Hussein akisema aliweza kukabiliana vyema na magaidi.
Bw Trump alikuwa akihutubia mkutano wa kampeni eneo jimbo la North Carolina Jumanne alioanza kuzungumza kuhusu kiongozi huyo aliyeuawa kwa kunyongwa Desemba 2006.
“Saddam Hussein alikuwa mbaya, kweli? … Lakini mnafahamu ni jambo gani aliweza kulifanya vyema sana? Aliwaua magaidi. Alifanya hivyo vyema sana,” Trump alisema.
“Hawakuwasomea haki zao, hawakunena lolote. Walikuwa magaidi, mambo yao kwisha.”
Bw Trump awali amewahi kusema kwamba ulimwengu ungelikuwa “asilimia 100 bora kuliko sasa” iwapo viongozi wa kiimla kama Saddam Hussein na kiongozi wa muda mrefu wa Libya Muammar Gaddafi wangelikuwa bado uongozini.
Kabla ya uvamizi ulioongozwa na Marekani, ambapo Saddam aliondolewa madarakani, Iraq ilikuwa imeorodheshwa na Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Marekani kama taifa linalofadhili ugaidi.
Image copyrightGETTYImage captionSaddam Hussein aliongoza Iraq kuanzia 1979 hadi 2003
Afisa mkuu mshauri wa Hillary Clinton kuhusu sera, amejibu matamshi ya Bw Trump kwa kusema kuwa: “Sifa za Donald Trump kwa viongozi wa kiimla yamkini hazina mipaka.”
Amesema matamshi kama hayo yanaashiria “ni jinsi gani itakuwa hatari (kuwa na Trump) kuwa Amiri Jeshi Mkuu na jinsi ambavyo hafai kuhudumu kama rais.
Image copyrightGETTY IMAGESImage captionTrump amesema ujumbe wake umefasiriwa visivyo
Mgombea urais wa chama cha Democratic nchini Marekani Hillary Clinton amesema ujumbe ulioandikwa na mpinzani wake Donald Trump kwenye Twitter ulieneza chuki dhidi ya Wayahudi.
Ujumbe huo wa mgombea huyo wa chama cha Republican ulikuwa na umbo linalokaribiana na nyota ya Daudi pamoja na rundo la pesa.
Ndani ya umbo hilo, kulikuwa na maandishi yaliyoeleza kuwa Bi Clinton ndiye “mgombea mfisadi zaidi kuwahi kuwepo!”
Ujumbe huo ulifuywa baadaye na badala yake akaandika ujumbe mwingine maandishi hayo yakiwa ndani ya umbo la duara.
Bw Trump alisema vyombo vya habari vina unafiki kwa kulinganisha umbo lake na umbo la Nyota ya Daudi, ishara ya Uyahudi.
Image copyrightMIC
"Hatua ya Donald Trump kutumia picha za chuki dhidi ya Wayahudi kutoka kwenye tovuti za kibaguzi kuendelea kampeni yake inashtua,” maafisa wa kampeni wa Bi Clinton walisema. “Lakini hali kwamba haya ni mazoea inafaa kuwatia hofu wapiga kura.”
Mwanamume mmoja raia wa Uingereza
anayetuhumiwa kwa kupora bunduki ya afisa mmoja wa polisi katika mkutano
wa kisaiasa wa Donald Trump, amewaambia wapelelezi wa Marekani kuwa,
alitaka kumuua kwa kumpiga risasi na kumuuwa mgombea huyo wa kiti cha
Urais wa chama cha Republican.
Kwa mjibu wa stakabadhi za
mahakama, Michael Sandford anasema kuwa aliendesha gari hadi Las Vegas
akiwa na nia ya kumpiga risasi Bw Trump siku ya Jumamosi.Awali Donald
Trump alimtimua Maneja wake wa kampeni Corey Lewandowski kwa kutofautana
naye katika kauli zake.
Makamu wa Rais wa Marekani Joe Biden amemlaum Trump kwamba kauli zake ni za hatari
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta
anafanya mazungumzo na kiongozi wa upinzani nchini humo Raila Odinga ili
kuondoa wasiwasi wakati ambapo taifa hlo linajiandaa kwa uchaguzi mwaka
mkuu ujao.
Bw Odinga alikatiza ziara yake ya kushiriki katika
mazishi kusini magharibi mwa eneo la Natol ili kuhudhuria mkutano huo wa
Uhuru Kenyatta katika mji mkuu wa Nairobi.
''Nilipokea simu
kutoka ikulu ya mkutano na rais Uhuru Kenyatta.Naomba ruhusa yenu watu
wa Narok nielekee kuzungumza naye,alinukuliwa na gazeti la Daily Nation
akiwaambia waombolezaji.Nitatangaza kwa Wakenya iwapo tumekubaliana na
iwapo hatujakubaliana pia nitawaelezea'', aliongezea bw Odinga. Muungano wa upinzani nchini Kenya Cord umeapa
kuhudhuria mkutano jijni Nairobi hapo kesho,licha ya kwamba serikali
ilitangaza kupigwa marufuku.
Watu kadhaa wameuawa katika ghasia kati ya polisi na wafuasi wa upinzani wanaopigania mabadiliko ya sheria ya kupiga kura.
Mgombea kiti cha Urais kwa tiketi ya
chama cha Republican nchini Marekani Donald Trump, amehutubia umati wa
waendesha pikipiki Jijini Washington.
Trumph ametoa hotuba hiyo katika maadhimishoya kuwakumbuka maafisa wa polisi wa kiume na wa Kike wa Marekani.
Amesema
watu walioko Marekani kinyume na sheria, wanahudumiwa vyema kuliko
maveteran wa kijeshi suala ambalo amesema halitaendelea katika utawala
wake.