Kamanda wa kundi la al-Shabaab
aliyejiunga na kundi linalojiita Islamic State nchini Somalia amekamatwa
na maafisa wa usalama nchini humo.
Vyombo ya habari nchini Somalia vinasema alikuwa anajificha katika mtaa huo kutoka wa wapiganaji wa al-Shabab.
Serikali ya Somalia ilikuwa imeahidi zawadi ya $2,000 kwa mtu ambaye angetoa habari za kusaidia kukamatwa kwake.
Kamanda huyo alijiunga na kundi la Islamic State mwishoni mwa mwaka 2015.
Serikali ya Somalia inamtuhumu kwa kuhusika katika mashambulio dhidi ya wanajeshi wa Somalia na vikosi vya Umoja wa Afrika (Amisom) mjini Mogadishu.
Post a Comment