Mahakama ya Kikatiba nchini Afrika
Kusini imeiamuru kampuni ya mawasiliano ya Vodacom kumlipa mwanamume
aliyebuni wazo la kutuma ujumbe wa kumuomba apigiwe simu.
Huduma hiyo humuwezesha anayetumia simu kutuma ujumbe bila malipo kwa wateja wengine akiwaomba wampigie simu.
Tovuti ya Tech Central ya Afrika Kusini inasema uamuzi wa kesi hiyo, ambayo imesikizwa tangu 10, itakuwa na athari kubwa.
Haijabainika Bw Makate atalipwa pesa ngapi na Vodacom.
Lakini awali amewahi kuambia Moneyweb kwamba uvumbuzi huo wake ulizalishia kampuni hiyo karibu randi 70 bilioni za Afrika Kusini ($5bn; £3bn) na alitaka alipwe 15% ya pesa hizo.
Post a Comment