Latest in Tech

Ethiopia yatekeleza operesheni Sudan Kusini

Serikali ya Ethiopia inasema kuwa wanajeshi wake wamelizingira eneo moja nchini Sudan Kusini ambapo inaamini zaidi ya watoto 100 waliotekwa nyara wanazuiliwa.

Watoto hao walitekwa katika uvamizi wa mpakani ijumaa iliopita,ambapo zaidi ya watu 200 waliuawa.
Ethiopia imesema kuwa itawavamia washambuliaji wanaodaiwa kutoka katika jamii ya Murle.

Washambuliaji hao wanadaiwa kuingia nchini Ethiopia kutoka Sudan Kusini na kuchukua mifugo na mara nyengine huwateka watoto.

Share this:

Post a Comment

 
Copyright © bakinamimi. Designed by OddThemes & VineThemes