Latest in Tech

Lucy Kibaki afariki

Lucy kibaki na mkewe wakati wa kampeni za uchaguzi mwaka 2007
 Aliyekuwa mke wa rais wa zamani nchini Kenya Lucy Kibaki amefariki.


Lucy Kibaki na mumewe Mwai KIbaki wakiwapungia mkono wafuasi wao mda mchache baada ya kibaki kuwasilisha stakhabadhi zake za uchaguzi katika tume ya uchaguzi mwaka 2007.Picha ni kwa niaba ya Getty images

 Lucy alifariki katika hospitali ya Bupa Cromwell mjini London. Alisafrishwa hadi mjini Landon wiki moja iliopita kwa matibabu.


Lucy Kibaki pamoja na aliyekuwa mke wa aliyekuwa rais wa Marekani George Bush ,Laura Bush.Picha kwa niaba ya Getty Images
 Akithibitisha kifo chake rais wa Kenya Uhuru Kenyatta amesema kuwa kenya imesikitishwa na kifo cha mama Lucy mke wa aliyekuwa rais wa Kenya Mwai Kibaki.

Lucy Kibaki na mumewe aliyekuwa rais wa Kenya Mwai Kibaki pamoja na mkewe marehemu Kijana Wamalwa wakati wa misa ya kifo cha Wamalwa.Picha kwa niaba ya Getty Images
Katika taarifa iliotumwa katika vyombo vya habari Uhuru amesema bi Lucy amekuwa mgonjwa kwa kipindi cha mwezi mmoja.
Amesema kuwa Kenya imempoteza mwanamke aliyechangia mengi katika maendeleo ya taifa la Kenya hususan katika vita dhidi ya ugonjwa wa ukimwi.
Rais ametuma risala za rambi rambi kwa mtangulizi wake Mwai Kibaki pamoja na familia yake.

Share this:

Post a Comment

 
Copyright © bakinamimi. Designed by OddThemes & VineThemes