By
Unknown
•
05:58:00
•
HABARI
MATUKIO
•
|
Lucy kibaki na mkewe wakati wa kampeni za uchaguzi mwaka 2007
|
Aliyekuwa mke wa rais wa zamani nchini Kenya Lucy Kibaki amefariki.
|
Lucy Kibaki na mumewe Mwai KIbaki
wakiwapungia mkono wafuasi wao mda mchache baada ya kibaki kuwasilisha
stakhabadhi zake za uchaguzi katika tume ya uchaguzi mwaka 2007.Picha ni
kwa niaba ya Getty images
|
Lucy alifariki katika hospitali ya Bupa Cromwell mjini London. Alisafrishwa hadi mjini Landon wiki moja iliopita kwa matibabu.
|
Lucy Kibaki pamoja na aliyekuwa mke wa aliyekuwa rais wa Marekani George Bush ,Laura Bush.Picha kwa niaba ya Getty Images
|
Akithibitisha kifo chake rais wa Kenya Uhuru Kenyatta amesema kuwa kenya
imesikitishwa na kifo cha mama Lucy mke wa aliyekuwa rais wa Kenya Mwai
Kibaki.
|
Lucy Kibaki na mumewe aliyekuwa rais
wa Kenya Mwai Kibaki pamoja na mkewe marehemu Kijana Wamalwa wakati wa
misa ya kifo cha Wamalwa.Picha kwa niaba ya Getty Images
|
Katika taarifa iliotumwa katika vyombo vya habari Uhuru amesema bi Lucy amekuwa mgonjwa kwa kipindi cha mwezi mmoja.
Amesema
kuwa Kenya imempoteza mwanamke aliyechangia mengi katika maendeleo ya
taifa la Kenya hususan katika vita dhidi ya ugonjwa wa ukimwi.
Rais ametuma risala za rambi rambi kwa mtangulizi wake Mwai Kibaki pamoja na familia yake.
SIMILAR ARTICLES
Post a Comment