Aliyekuwa rais wa shirikisho la soka
duniani FIFA Sepp Blatter ameelezea vile maafisa wa serikali ya Uswizi
walivyomtaka kumsihi rais wa Burundi anayependa soka Pierre Nkurunziza
kujiuzulu kufuatia maandamano dhidi ya uongozi wake mwaka
uliopita,kulingana na jarida la soka duniani.
Mnamo mwezi Mei ,waziri wa kigeni wa Uswizi Yves Rossier alimtaka Sepp Blatter kumpatia Nkurunziza kazi ya ubalozi wa soka kulingana na jarida hilo.
Bwana Rossier alifanya ombi hilo baada ya kuagizwa na Marekani,lakini mpango huo ukafeli kwa sababu alikuwa na maswala mengine yaliokuwa yakimkabili,bwana Blatter alinukuliwa akisema.
Post a Comment