Polisi wa kupambana na ufisadi
nchini Nigeria, wamenasa saa ya thamani ya takriban dola milioni moja
kutoka kwa nyumba ya waziri wa zamani wa mafuta anayechunguzwa kwa
ufisadi.
Shirika la kupambana dhidi ya ufisadi la Nigeria (Economic and Financial Crimes Commission) limeithibitishia BBC kuwa bi Madueke anachunguzwa kufuatia madai ya ufisadi.
Mabilioni ye fedha zilitoweka katika wizara hiyo akiwa mamlakani.
Mwaka uliopita bi Madueke alikamatwa na kuhojiwa na maafisa wa upelelezi wa Uingereza lakini akaachiwa kwa dhamana.
Rais mpya wa Nigeria Muhammadu Buhari alichaguliwa kwa nia ya kumaliza kabisa ufisadi uliokuwa umekithiri nchini humo.
Rais Muhammadu ameahidi kutokomeza kabisa ufisadi.
Post a Comment