Maelfu ya wanaharakati walikutana
katika bunge la North Carolina siku ya Jumatatu ambalo likikutana kwa
mara ya kwanza tangu lipitishe sheria inayokosolewa kuwa dhidi ya
wapenzi wa jinsia moja.
Zaidi ya wakosoaji 50 wa sheria hiyo walikamatwa baada ya kuingia na kukataa kutoka katika jengo hilo.
Sheria hiyo yenye utata inatetea sheria inayowabagua watu wa jinsia moja.
Pia inawataka watu wa jinsia hiyo kutumia misala kulingana na vibali vya jinsia ya kuzaliwa.
Kampuni kubwa kama vile Benki ya Marekani na Apple zimekosoa sheria hiyo.
Post a Comment