Mshindi wa shindano la Big Brother Africa 2014, Hotshots Idris Sultan,
amevunja ukimya na kuzungumzia tetesi ambazo zilikuwa zinazagaa kwenye
mitandao ya kijamii kwamba kuna mtu alimpatia pesa zake kwa ajili ya
biashara lakini akazitumia vibaya kinyume na makubaliano.
Ikumbukwe mshindi huyo wa Big Brother Africa 2014, alipata zaidi ya
milioni 500. Pesa ambayo alidai aliitumia kuwekeza katika biashara
mbalimbali, na baadae aliweka wazi kwamba pesa hizo zilishaisha.
“Kuna watu ambao nimeweza kufanya nao kazi, lakini wakaaribu baadhi ya
mambo, nisingependa kuliongelea kwa sababu kuna baadhi ya vitu ambavyo
wameviharibu sana, na hawakuweza kuviweka sawa,” alisema Idris.
Aliongeza, “Yaani kama kupunyua, hivi vitu vinatokeaga katika sehemu
yoyote, kwenye kampuni, kwenye nini. Kuna watu wanaweza wakafuja mali
zako au wakafanya vitu vibaya kinyume na mlivyo kubaliana. Kwa hiyo siyo
inshu kubwa sana kwangu, kwa sababu maisha yanaendelea na milango
inafunguka,”
Stori ambazo zilikuwa katika mitandao ya kijamii zilikuwa zinadai kuwa
meneja wa zamani wa Idris, ndiye ambaye alimwingiza mkenge Idris, kitu
ambacho Idris hakupenda kukizungumzia zaidi.
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
Post a Comment