![]() |
| Dilma Rousseff |
Rais wa Brazil Dilma Rousseff ameshtumu hatua ya kumshtaki kuwa ''mapinduzi na mchezo'' akikana kutekeleza uhalifu wowote.
Bi Rousseff amesema kuwa serikali yake inahujumiwa.
Makamu wa rais Michel Temer atakuwa kaimu rais huku kesi ya Roussef ikiendelea.
Kesi hiyo huenda ikachukua takriban siku 180,ikimaanisha kwamba bi Roussef hatosimamia michezo ya Olimpiki itakayofanyika mjini Rio de Janeiro,ambayo inaanza mwezi Agosti tarehe 5.
Maseneta walipiga kura ya kumsimamisha kazi kwa kura 55 dhidi ya 22 baada ya kikao cha usiku kucha kufanyika kwa saa 20.
Katika hotuba yake ,bi Rousseff amesema kuwa huenda alifanya makosa lakini hakutekeleza uhalifu wowote,''sikukiuka sheria za bajeti''.
Alisema:Kile kilichopo ni heshima na uhuru wa wapiga kura na katiba ya raia wa Brazil.


Post a Comment