Mshambuliaji wa Leicester Jamie Vardy ametawazwa mchezaji soka bora wa mwaka na chama cha waandishi wa kandanda Uingereza.
Vardy, 29, amefunga mabao 22 Ligi ya Premia msimu huu.
Aidha, alivunja rekodi kwa kufunga mabao kila mechi katika mechi 11 mtawalia.
Klabu yake inahitaji alama mbili pekee kushinda Ligi Kuu ya Uingereza lakini inaweza pia kutawazwa mabingwa iwapo Tottenham watashindwa kuwalaza Chelsea jioni.
Mahrez alishinda tuzo ya mchezaji bora wa mwaka ya PFA, ambayo mshindi hupigiwa kura na wachezaji soka ya kulipwa, mwezi jana.
Post a Comment