Home » UCHUMI » WAFAHAMU NA KUWAJUA MARASI WANAOONGOZA KWA UTAJIRI AFRIKA
WAFAHAMU NA KUWAJUA MARASI WANAOONGOZA KWA UTAJIRI AFRIKA
arida la kiuchumi la Forbes limetoa orodha ya viongozi wanane barani
Afrika ambao limewataja kuwa ndio wanasiasa matajiri zaidi barani humo.
Kwa mujibu wa jarida hilo la Marekani, Rais José Eduardo dos Santos wa
Angola anaongoza katika orodha hiyo akiwa na utajiri wenye thamani ya
dola bilioni 20 na hivyo kuhesabiwa kuwa, kiongozi tajiri zaidi barani
Afrika. Rais do Santos amekuwa madarakani nchini Angola kwa miaka 34
sasa. Wakati rais wa Angola akiongoza kwa kuwa Rais wenye utajiri mkubwa
zaidi barani Afrika, asilimia 70 ya wananchi wake wanaishi katika
umasikini. Kwa mujibu wa orodha ya jarida hilo la Forbes, Mfalme
Muhammad VI wa Morocco anashika nafasi ya pili kwa kuwa na utajiri wenye
thamani ya dola bilioni 2.1, Rais Teodoro Obiang Nguema Mbasogo wa
Equatorial Guinea anashika nafasi ya tatu katika orodha hiyo kwa kuwa na
utajiri wa dola miloni 600. Aidha kwa mujibu wa ripoti hiyo, Rais Uhuru
Kenyatta wa Kenya anashika nafasi ya nne akiwa na utajiri wa dola
milioni 500. Wengine walioko katika orodha hiyo ya viongozi wanane
matajiri barani Afrika ni Rais Paul Biya wa Cameroon dola milioni 200,
Mfalme Mswati III wa Swaziland dola milioni 100, Rais Idriss Deby wa
Chad dola milioni 50 na Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe mwenye utajiri wa
dola milioni 10.
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
Post a Comment