Latest in Tech

Zlatan Ibrahimovic amjibu Eric Cantona

Mshambuliaji mpya wa Manchester United, Zlatan Ibrahimivic amemjibu nyota wa zamani wa soka, Eric Cantona kutokana na kauli yake ya siku chache zilizopita iliyodai kuwa mchezaji huyo hawezi kuwa mfalme ndani ya timu hiyo labda achague kuwa mtoto wa mfalme.
zlatan-ibrahimovic-manchester-united_3493668
“Just one last thing, there can only be one King in Manchester. You can be the Prince if you want to. And the No 7 is yours if you are interested. That is my welcome gift to you… The King is gone! Long live the Prince!,” ulikuwa ni ujumbe alioutoa Cantona siku chache zilizopita.
Baada ya kauli hiyo, Ibrahimovic ameliambia gazeti la Aftonbladet, “I admire Cantona and I heard what he said.”
“But I won’t be King of Manchester. I will be God of Manchester,” ameongeza.
Wachezaji hao wote wawili wanajulikana kuwa na sifa ya utukutu huku Cantona aliondoka United akiwa hana maelewano mazuri na aliyekuwa kocha wake Ferguson na Ibrahimovic naye aliwahi kukwaruzana na Pep Guadiola wakati wapo Barcelona lakini pia aliwahi kufungiwa kwa kosa la kumpiga muamuzi.

Share this:

Post a Comment

 
Copyright © bakinamimi. Designed by OddThemes & VineThemes