Latest in Tech

Magufuli ateua makatibu tawala wa mikoa Tanzania

Rais wa Tanzania Dkt John Magufuli amefanya mabadiliko katika makatibu watawala wa mikoa, makatibu kumi wakiwa wapya.
Wawili wamebadilishiwa vituo vya kazi na 13 wamesalia katika vituo vyao vya sasa.
Makatibu tawala wapya walioteuliwa, na ambao wataapishwa Jumatano wiki hii, ni:
  1. Arusha - Richard Kwitega
  2. Geita - Selestine Muhochi Gesimba
  3. Kagera - Armatus C. Msole
  4. Kilimanjaro -Mhandisi Aisha Amour
  5. Pwani - Zuberi Mhina Samataba
  6. Shinyanga - Albert Gabriel Msovela
  7. Singida - Dkt. Angelina Mageni Lutambi
  8. Simiyu - Jumanne Abdallah Sagini
  9. Tabora - Dkt. Thea Medard Ntara
  10. Tanga - Mhandisi Zena Said
Makatibu Tawala waliobadilishwa vituo vya kazi ni;
  1. Kigoma - Charles Amos Pallangyo (Kutoka Mkoa wa Geita)
  2. Morogoro - Dkt. John S. Ndunguru (Kutoka Mkoa wa Kigoma)
Makatibu Tawala waliobakishwa katika vituo vyao vya sasa vya kazi ni;
  1. Dar es salaam - Theresia Louis Mbando
  2. Dodoma - Rehema Hussein Madenge
  3. Iringa - Wamoja Ayubu Dickolagwa
  4. Katavi - CP Paul Chagonja
  5. Lindi - Ramadhan Habibu Kaswa
  6. Mara - Benedict Richard Ole Kuyan
  7. Manyara - Eliakimu Chacha Maswi
  8. Mbeya- Mariam Amri Mjunguja
  9. Mtwara - Alfred Cosmas Luanda
  10. Mwanza - CP. Clodwing Mathew Mtweve
  11. Njombe - Jackson Lesika Saitabau
  12. Rukwa - Symthies Emmanuel Pangisa
  13. Ruvuma - Hassan Mpali Bendeyeko

Share this:

Post a Comment

 
Copyright © bakinamimi. Designed by OddThemes & VineThemes