Latest in Tech

Mazungumzo kuhusu Burundi kufanyika Tanzania

Watu karibu 500 wameuawa nchini Burundi tangu Aprili mwaka jana
Rais wa zamani wa Tanzania Benjamin Mkapa ametangaza kwamba kikao cha kwanza cha mazungumzo ya kutafuta amani nchini Burundi kitafanyika wiki ijayo.

Bw Mkapa aliteuliwa na Jumuiya ya Afrika ya Mashariki mapema mwezi uliopita kuwa mfanikishi wa mazungumzo ya kutatua mzozo wa kisiasa katika taifa hilo la Afrika Mashariki.

Rais wa Uganda Yoweri Museveni alisalia kuwa mpatanishi mkuu.

Mazungumzo ya kutafuta amani yalifeli mwishoni mwa mwaka jana baada ya upande wa serikali kusema hauwezi kuzungumza na watu waliohusika kwa njia moja au nyingine katika jaribio la mapinduzi la mwezi Mei mwaka jana.
Bw Mkapa ameandika kwenye Twitter kwamba wadau wote wanatarajia kuhudhuria kikao cha kwanza cha mazungumzo ambacho kitafanyika mjini Arusha kuanzia tarehe 2 Mei hadi 6 Mei.

"Nimepata idhini kutoka kwa Rais wangu, kiao changu cha kwanza cha Mashauriano ya Burundi kitakuwa mjini Arusha,” aliandika.

Ukosefu wa usalama umeendelea kuwa tatizo kuu nchini Burundi na visa vya watu kuuawa kiholela vimekuwa vikiripotiwa mara kwa mara

Share this:

Post a Comment

 
Copyright © bakinamimi. Designed by OddThemes & VineThemes