Rais Obama ameanza ziara rasmi
Ujerumani, akiwa na lengo la kuzungumzia mkataba wa kibiashara
unaopendekezwa, baina ya Marekani na bara la Ulaya, uitwao T-TIP.
Hapo jana, maelfu ya watu waliandamana, katika mji wa Hanover, kupinga mkataba huo.
Rais Obama atakuwa mjini humo kwa siku mbili zijazo.
Rais Obama anasema mkataba huo utaleta ajira na kukuza uchumi.
Lakini muandishi wa BBC mjini Berlin, anasema atakuwa na kazi pevu ya kushawishi watu wakubaliane naye.
Post a Comment