Beyoncé alishangaza wengi jumatatu hii baada ya
kutokea kwenye usiku wa Met Gala bila mume wake Jay Z. Ikiwa bado zile
tetesi za usaliti zinakiki sana baad aya album ya Lemonade, kutoka basi ilisemekana labda hio ndio sababu.
Mtu wa karibu na Beyoncé na Jay Z amesema wawili
hawa wako powa kabisa na hakuna tatizo lolote kati yao, kuhusu Jay Z
kutoonekana kwenye Met Gala, alifunguka kuwa sio kawaida ya Jay Z
kuonekana kwenye sehemu kama hizo.
Alisema “Wasanii
wanaoenda huko wanakitu tayari sokoni cha kusukuma sio kwenda tu,Jay Z
hana kazi mpya kwa sasa ,aende kufanya nini, ndio maana unaona kila
aliyekuwepo ana album au movie mpya kwa sasa“.


Post a Comment