Akiwa kwenye mahojiano na DJ Drama kwenye kipindi cha ‘Shade 45’
radio ya “Streetz Is Watchin Radio” rapa Lil Wayne amefunguka kiasi cha
pesa ambacho Jay Z alitaka kumpa ili kujiunga na Roc-A-Fella.
Lil Wayne anasema “Jay Z nilikutana
naye kuhusu kujiunga na Roc-A-Fella [Records], akiwa club 40/40 na
kupiga stori kama tunajuana, Jay Z alinipa ofa ya dola laki moja na elfu
sabini na tano [175 thousand dollars] na nilivyosikia kiasi hicho
nilicheka sana na kupiga mahesabu na kugundua pesa hizo hata hazifiki
thamani ya meno yangu mawili mdomoni, tulicheka na ndio hivyo”.
Kuhusu album na muziki mpya Wayne kasema anasubiri matatizo yake ya lebel kumalizika.
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
Post a Comment