Klabu ya soka ya Atletico Madrid
imefanikiwa kutinga fainali ya klabu bingwa barani Ulaya kwa mara ya
pili ndani ya kipindi cha miaka mitatu baada ya kupata bao la ugenini
walipokipiga dhidi ya Bayern Munich ya Ujerumani.
Mlinda mlango wa Atletico Jan Oblak aliokoa mkwaju wa penalti uliopigwa na Thomas Muller kabla ya mshambuliaji Antoine Griezmann kusawazisha na kuwa 1-1.
Matokeo ya jumla ya nusufainali hiyo yalimalizika sare 2-2 lakini Madrid wakasonga kwa kuwa na bao la ugenini.
Sasa Atletico watakutana na mshindi wa mchezo kati ya Real Madrid na Manchester City utakaopigwa kesho dimbani Santiago Bernabeu katika fainali mjini Milan tarehe 28 Mei.


Post a Comment