Latest in Tech

BASATA YAMPIGA MARUFUKU SNURA KUTOJIHUSISHA NA SANAA

Wizara ya Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo leo imetangaza rasmi kumfungia msanii wa bongo fleva Snura kujihusisha na masuala ya sanaa. Mkuu wa Kitengo cha mawasiliano wa Wizara ya Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo, Zawadi Msalla ameongea na waandishi wa habari na kuthibitisha taarifa hizi.

Wimbo huu wa Chura umefungiwa kupata muda wa hewani kwenye redio na TV nchini. Taarifa hiyo imetolewa na wizara hiyo kwenye mkutano na waandishi wa habari uliofanyika kwenye ukumbi wake wa mikutano wizarani hapo  Dar es salaam.

Uamuzi wa kumfungia umekuja kutokana msanii huyo kutojisajili kwenye Baraza la Sanaa la Taifa, BASATA.

Share this:

Post a Comment

 
Copyright © bakinamimi. Designed by OddThemes & VineThemes