Aliyekuwa winga wa klabu ya Manchester united ‘Ryan Giggs’ ametengana
na mke wake Stacey baada ya tuhuma kuwa Giggs ameanza tena tabia yake
ya kumsaliti na wanawake tofauti.
Tuhuma hizi zimeibuka tena baada ya ukaribu wa kimapenzi wa Giggs na
mfanya kazi wake wa kike kwenye mgahawa wake uliopo mjini Manchester.
Giggs na mke wake walifunga ndoa September 2007,katikati hapa Gigs
alihusishwa kumsaliti mke wake na wanawake kama model Imogen Thomas na
mke wa mdogo wake Natasha Lever ila alitumia nguvu na pesa kuzuia stori
hizi kusamba kitu ambacho kilishindikana kwa asilimia 100.
Taarifa mpya zinasema mke wa Giggs anataka talaka yake sasa.
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
Post a Comment