Latest in Tech

BAYERN BIGWA LIGI KUU UJERUMAN 'BUNDESLIGA'

Bayern Munich imeishinda Borussia Dortmund kwa penalti 4-3 na kubeba ubingwa wa Kombe la Ujerumani.

Huo ni ushindi wa 11 kwa Bayern kushinda makombe mawili ya Bundesliga na Kombe la Ujerumani kwa wakati mmoja.


Lakini klabu hiyo, imemuaga vizuri kocha Pep Guardiola ambaye alishindwa kujizuia na kumwaga chozi. Kocha huyo anaondoka na kwenda kujiunga na Manchester City.

Timu hizo zilicheza kwa dakika 120 bila kupata mshindi na zikalazimika kupigiana mikwaju ya penalti.

Kipa nyota wa Bayern, Manuel Neuer aliokoa mkwaju ya Sven Bender na Sokratis Papastathopoulos akakosa.

Kipa mzoefu wa Dortmund, Roman Buerki aliokoa mkwaju wa Joshua Kimmich lakini Thomas Muller akafunga na kuifanya Bayern iendelee kubaki kwenye msitari.






Share this:

Post a Comment

 
Copyright © bakinamimi. Designed by OddThemes & VineThemes