Latest in Tech

MICHEZO

SIASA

VIDEOS

Latest Updates

MAMBO 10 MUHIMU YA KUZINGATIA UKIWA NA MTOTO CHINI YA MIAKA MITANO

00:37:00
                                                           
                                                                                           
wanaawake wengi wakishajifungua hupenda kuishi kwa mazoea au uzoefu hasa kwa kufuata bibi na mama wanasema nini kuhusu afya ya mtoto, sio vibaya lakini ni vizuri uwe makini sana kwani maisha yamebadilika sana na kuna mambo mengi yamepitwa na wakati na mengine ni hatari kiafya hivyo usikubali kila unachoambiwa na watu bila kukichuja.
kuna mambo kadhaa ya msingi sana ambayo usipokua makini nayo utampoteza mtoto kama ifuatavyo.
hakikisha anapata chanjo zote; ukiona unaambiwa mtoto anatakiwa achomwe chanjo fulani maana yake ugonjwa unaozuiliwa na chanjo hiyo umeshaua watoto wengi sana hivyo ukileta uzembe tu mtoto wako anaweza kua mmoja wa watakao uwawa na ugonjwa huo.
mpeleke hospitali akiugua; mara nyingi akina mama hunza kutibu wenyewe na wakiona mtoto amezidiwa kabisa ndio wanakimbia hospitali, mara nyingi watoto hawa wanapona kwa bahati tu lakini wengi hufariki..mtoto sio kama mtu mzima akiugua kidogo tu anafariki hivyo usilete uzembe katika hili.
tumia neti ya mbu; kama wewe neti huiwezi basi nunua kitanda maalumu cha mtoto usiku akilala alale na net, malaria inaongoza kwa kuua watu hapa afrika na watoto wakiuawa zaidi kuliko hata watu wazima.
kula vizuri mlo kamili; ili upate maziwa ya kutosha yenye virutubisho vyote hakikisha unakula vizuri kwa kufuata mlo kamili yaani mchanganyiko wa vyakula vyote, kipindi mtoto ananyonya achana na mawazo ya kupungua uzito, subiri afikishe miaka miwili ya kunyonya ndio uanze kupungua lakini pia mifupa, nyama na kila kitu cha mtoto kinatokana na wewe hivyo kula vizuri kurudishia madini yaliyopotea wakati wa ujauzito...usipozingatia hili utakutana na upungufu wa madini siku za usoni
osha matiti yako kila ukitaka kunyonyesha; akina mama wengi wana shughuli nyingi hatukatai lakini tabia ya kunyonyesha bila kuosha matiti wakati wa shughuli hizo ndio chanzo cha mtoto kuharisha mara kwa mara. ukitoka kwenye shughuli zako oga au osha matiti afu ndio umpe mtoto anyonye.
fuata ushauri wa daktari; usipende kutoa dawa hovyo bila kupata ushauri wa daktari au muhudumu wa afya, dawa hizo hutolewa kwa uzito na mara nyingi uzito wa mtoto huongezeka kila mara hivyo dozi aliyopewa miezi mitatu iliyopita huenda mwezi huu haimtoshi tena.
achana na maziwa mbadala; kama hauna jinsi labda wewe ni muathirika wa ukimwi na umekatazwa kunyonyesha au hauna maziwa ya kutosha basi unaweza kumpa mtoto maziwa ya ngombe au maziwa ya dukani lakini nikuthibitishie kwamba maziwa ya mama hayana mbadala wa 100%, yale ya mama ni bora zaidi kwa afya ya mwili na akili za darasani hapo baadae.
weka hatari zote mbali na mtoto; mtoto asipelekwe jikoni kwenye moto, usiweke dawa zozote mahali pa wazi yaani dawa za panya, dawa za binadamu na kadhalika, nyumba yako hakikisha haina shimo hata moja na hakikisha mtoto hachezi barabarani yaani hatari zote weka mbali.
simamia maendeleo ya mtoto; baadhi ya wanawake wako bize sana na maisha baada ya kujifungua hivyo kazi ya kulea huwaachia wafanyakazi wa ndani, ni hatari sana kukabidhi maisha ya mtoto wako kwa mfanyakazi..jitahidi uende clinic hata mara moja moja ujue maendeleo yakoje, jifunze jinsi ya kusoma kadi ya clinic kujua kama uzito unapanda au unashuka, rudi nyumbani ghafla ukague kama mtoto anapewa chakula kama unavyotaka.
kua makini usibebe mimba mpya kabla huyo mdogo hajakua; kunyonyesha tu kunaweza kuzuia mimba lakini kama mama ananyoshesha zaidi ya mara kumi kwa siku ndani ya miezi sita ya kwanza kama huwezi kutumia kalenda au damu hazijaanza kutoka basi chagua njia ya uzazi wa mpango ambayo ni salama kwa mtoto.

NJIA 10 ZA KUJITIBU UCHOVU WA POMBE {HANGOVER}

23:49:00

hangover ni nini?
hii ni hali ya kujisikia vibaya inayowapata watu watu ambao wanakua wamekunywa pombe nyingi jana yake, dalili zake ni kuuma kichwa sana, kutapika, kuishiwa nguvu, kujisikia uvivu sana na kushindwa kufanya kazi.
hali hii huvumilika mara nyingi lakini wakati mwingine hali hua mbaya kiasi kwamba mtu huweza kulazwa hospitali kwa matibabu zaidi.
sasa wewe kama mywaji wa pombe ni vizuri ukazifahamu njia ambazo unaweza kuzitumia kutibu hangover kabla au baada kunywa pombe kama ifuatavyo.
kunywa maji mengi;maji ni matibabu makuu ya hangover kabla na baada ya kunywa pombe, kawaida pombe humfanya mtu akojoe sana na kupoteza maji mengi mwilini na hii ndio moja ya sababu kuu ya kupata hangover sasa kitaalamu ili kuzuia hangover unatakiwa unywe chupa moja ya pombe na glass moja ya maji kila wakati na ikitokea hukufanya hivo na umeamka asubuhi una hangover basi jitahidi unywa hata lita tatu mpaka nne siku hiyo.[angalizo;usinywe maji yote kwa pamoja, weka kwenye chupa unywe taratibu]

kula chakula chenye mafuta mengi kabla ya pombe; chakula kama nyama, samaki, kuku, sambusa na vingine hua na mafuta mengi...pombe ikikuta mafuta tumboni inapata tabu kufanya kazi haraka kuliko ikikuta tumbo halina kitu, hii huzuia hangover za kesho yake lakini ukishakunywa haikusaidii tena.
kunywa kahawa; kawaha kitaalamu inaitwa stimulant, hii ni nzuri kwako ambaye umeamka na hangover lakini una kazi za kufanya siku hiyo zinazohitaji umakini mkubwa hivyo kahawa itakuondolea uchovu na kukufanya uwe makini lakini kunywa na maji pia kwani kahawa hufanya mtu akojoe sana kama pombe.
meza dawa za maumivu; maumivu ya kichwa yakiwa makali kuna dawa unaruhusiwa kumeza kupunguza maumivu hayo mfano diclofenac, aspirin, ibuprofen...usinywe paracetamol au dawa yeyote yenye mchanganyiko wa paracetamol kwani ikiungana na pombe inaharibu maini
                                                             
fanya mazoezi; kama kichwa hakiumi sana fanya mazoezi yeyote kwani hii itakusaidia kupunguza pombe mwilini, na kukuletea mood ya kufanya vitu kwani ubongo hutengeneza homoni ya furaha yaani endorphine wakati wa mazoezi.
epuka kuzimua na pombe; huu msemo hutumika na walevi kwamba anaamka na pombe ili kuondoa pombe, hapana hii haifai kabisa kwani inaweza kukuletea ganzi mwilini na kukufanya uwe mtegemezi wa pombe kwenye maisha yako yaani bila kunywa pombe huwezi kufanya chochote.
                                                 
ongeza sukari mwilini;pombe hupunguza sana sukari mwilini na hii ni kwasababu maini
yanashindwa kutengeneza sukari ya ziada na kua bize kuondoa pombe mwilini hivyo unaweza kunywa juisi, soda au kula chakula. juice ni nzuri zaidi kwani hurudisha na madini yaliyopotea mwilini.
kunywa tangawizi na maji ya moto; chukua tangawizi isage kisha ichemshe na maji ya moto, hii itakuondolea kichechefu na kukuletea hamu ya kula.
rudi kulala; mara nyingi pombe huharibu mfumo wa usingizi hivyo mtu anaweza asipate usingizi wa kutosha kwa kushtuka ovyo usingizini, lala mpaka utakapoona usingizi umeisha ndio uanze shughuli zingine.
jiuepushe na mwanga mkali na sauti kubwa za kelele; mtu akiwa katika hali hii hawezi kuvumilia mwanga mkali na sauti kubwa hivyo kaa mbali navyo kupata nafuu.
                                                       

Huu ndo ujio mzito na mpya wa Ray C kimuziki

08:03:00





Kutoka Kushoto: Anna Peter wa East Africa Radio, Ray C na Mamy Baby wa Clouds FM

Miaka minne iliyopita, kwa hali aliyokuwa nayo, kila mtu alimkatia tamaa kuwa ndio basi tena ameshatumbukia kwenye shimo waliloshindwa kutoka vijana wengi. Matumizi ya madawa ya kulevya yalimuongezea jina la uteja lililolifunika jina lake la utani ‘kiuno bila mfupa.’ Rehema, msichana mrembo aliyekuwa ndoto ya wanaume wengi, akapoteza thamani yake.
Jina lake likapotea kwenye ramani ya muziki na akawa mtu wa kuonewa huruma. Na kwa jinsi madawa ya kulevya yalivyo, humnyong’onyeza mtumiaji, humpunguzia utimamu wake kiakili, humpa utegemezi unaotesa yasipotumiwa na ikawa wakati mwingi Rehema akawa wa kukutwa amezima! Maskini wa Mungu Ray C akaingia kwenye dimbwi la maji ya moto ya uteja, nani wa kumuokoa?
Kwa alama aliyoiweka kwenye muziki wa Tanzania kwa nyimbo kibao zilizofanya vizuri, Ray C akapata msaada kutoka kwa mtu mwenye cheo kikubwa zaidi nchini, Rais Jakaya Kikwete. Alijitolea kumpeleka rehab, kumsadia kwa hali na mali hadi hali yake ikarudi kwenye mstari – walau kwa muda huo. Aliingia kwenye mpango wa kutumia methadone aliodumu nao kwa takriban miaka mitatu.
Katika kipindi hicho, Ray C akageuka kuwa kinara wa vita dhidi ya matumizi ya madawa ya kulevya. Alianzisha pia taasisi yake, The Ray C Foundation kwaajili ya kampeni za kukemea ubwiaji unga. Katika kipindi hicho, Rehema, alijaribu tena kurejea kwenye muziki kwa kuachia wimbo mmoja ‘Mshum Mshum’, ambao hata hivyo haukufanikiwa kumrudisha pale alipokuwa ameishia.
Haikuwa rahisi kuishinda vita hiyo na mwaka huu alionekana kuweka silaha chini kwa kudaiwa kurejea tena kwenye matumizi ya madawa hayo. Video iliyosambaa mtandaoni akionekana akiwa kwenye mvurugano wa akili, akilia na kutaka kujichoma kisu, ilirejesha tena hofu kwa wapenzi wa muziki kuwa amerudi kwenye jela ya uteja.
RAY C ANARUDI
Peleka mbele hadi wiki moja iliyopita, Ray C anaonekana kupata chaji ya muziki inayompeleka hadi kwenye studio za kisasa za Wanene Entertainment. Kwanza nimefurahi kuona amebadilika mno kutoka yule msichana aliyenenepa hadi kuupoteza utambulisho wake. Amerudisha umbo lake la zamani linalompa matumaini ya kulikomboa jina la jukwaani – kiuno bila mfupa.

Uhakika nimeupata kwenye video alizoziweka Instagram zikimuonesha akiwa kwenye mazoezi makali ya kucheza huku kiuno chake kikifuata vyema maagizo kinayopewa. Huu unaweza kuwa urejeo wenye nguvu zaidi wa muimbaji huyu na namuomba Mungu amsaidie kukaa tena kwenye nafasi yake.
Muziki wa Tanzania unamhitaji Ray C hasa kwakuwa kuna upungufu wa wasanii wakubwa wa kike. Inanipa moyo kuona mahaba yake ya muziki yamerudi kwa kasi ya ajabu. Napata amani nikimuona anavyofurahia mchakato wa kutengeneza nyimbo mpya. Nafarijika kuona kuwa amezungukwa na watu wanaotaka arudi kwenye chati.
Atakachohitaji baada ya hapo ni kuungwa mkono na vituo vyote vya redio nchini na pia mashabiki wakitimiza wajibu wao. Yapaswa kukumbuka kuwa muziki pekee ndio unaweza kuwa mkombozi kwake na unaoweza kumpa nafasi ya pili – nafasi ya kung’ara tena.
Naamini anarekodi nyimbo nyingi na katika hizo lazima kutakuwa na nyimbo kubwa. Pamoja na matatizo yote aliyoyapita, sijawahi kuwa na shaka na kipaji chake. Nasubiri kwa hamu kusikia kile alichotuandalia.

UFC 202: Conor McGregor amcharaza Nate Diaz, pambano latawaliwa na damu (Picha)

11:41:00
Bondia Conor McGregor ameibuka mshindi dhidi ya Nate Diaz kwenye pambano la UFC 202 lililofanyika wikiendi hii.
377405E000000578-3751207-image-a-3_1471757130370
Ushindi huo ni kisasi cha McGregor dhidi ya Diaz aliyemshinda kwenye pambano lao lililopita.
Mahasimu hao walikumbatiana baada ya pambano kuisha na kushuhudia Diaz akienda chini mara tatu.
37740FA900000578-3751207-image-m-132_1471755171312
Diaz alionekana kuumizwa zaidi kwenye pambano hilo huku uso wake ukijaa damu. Diaz ametaka pambano la tatu.
Tazama picha zaidi:
3773F89500000578-3751207-image-m-66_1471752266117
37740AE100000578-3751207-image-m-129_1471755119674
37740FBD00000578-3751207-image-m-128_1471755105138
37741A1A00000578-3751207-image-a-6_1471757397940
377414EB00000578-3751207-image-a-34_1471758175828
377417FB00000578-3751207-image-a-31_1471758006073
3774000C00000578-3751207-image-m-74_1471752534111
3774059C00000578-3751207-image-m-83_1471753561111
3774109D00000578-3751207-image-a-12_1471757580572
3774156C00000578-3751207-image-a-15_1471757712379

VIDEO: TAZAMA UWEZO WA RAPA HUYU WA KIKE MWENYE UMRI WA MIAKA 13 ALIYESAINI SONY MUSIC

11:27:00
Lebo kubwa ya muziki Epic/Sony records wamefanya usajili mkubwa wiki hii baada ya kupata saini ya rapa Luis Rivera Jr Aka Lil Poopy mwenye miaka 13.

Lil Poopy alikuwa msanii wa French Montana kwenye kundi lake la Coke Boys na kutoa mixtape iliyopewa jina “Coke Aint A Bad Word“.
Album hii ilileta matatizo kwenye familia ya Lil Poopy na baba yake mzazi kuchunguzwa na polisi baada ya mtoto wake mwenye miaka 13 kuimba kuhusu Wanawake, dawa za kulevya ,ngono na magari ya thamani.

Msanii huyu anafananishwa na wasanii kama Bow wow,Lil Romeo na Taylor Swift walioanza muziki wakiwa wadogo.

Hii ndo list ya wasanii wanaotajwa kuwania tuzo za BET Hip-Hop 2016

06:04:00
Tuzo za hiphop za BET ziko njiani na tayari wametangaza wasanii wanaowania tuzo hizi kwenye vipengele tofauti, Kwa miaka mitatu mfululizo Drake ametajwa kuongoza kwenye vipengele vingi zaidi anavyowania msanii yoyote, Drake anawania tuzo kwenye vipengele 14 ambavyo ni kama Album of the Year, Track of the Year,na MVP of the Year.
Msanii Future anawania vipengele 10 ambavyo ni kama Album of the Year, Best Mixtape, na Made-You-Look Award kwa Best Hip-Hop Style.
DJ Khaled anawania vipengele 9 na Kanye West 8.
BET Hip-Hop Awards zinafanyika jumamosi ya  Sept. 17 kwenye ukumbi wa Cobb Energy Performing Arts Centre mjini Atlanta,na kuonekana kwenye tv Oct. 4
Orodha kamili ndio hii ya tuzo za BET Hip-Hop 2016.
Best Hip-Hop Video
2 Chainz – “Watch Out”
Desiigner – “Panda”
DJ Khaled feat. Jay Z & Future – “I Got the Keys”
Drake – “Hotline Bling”
Fat Joe & Remy Ma feat. French Montana & Infared – “All the Way Up”
Kanye West feat. Rihanna – “Famous”
Best Collabo, Duo or Group
DJ Khaled feat. Drake – “For Free”
DJ Khaled feat. Jay Z & Future – “I Got the Keys”
Drake & Future – “Jumpman”
Drake feat. Wizkid & Kyla – “One Dance”
Fat Joe & Remy Ma feat. French Montana & Infared – “All the Way Up”
Best Live Performer
Drake
Future
J. Cole
Kanye West
Kendrick Lamar
Lyricist of the Year
Chance the Rapper
Drake
J. Cole
Kanye West
Kendrick Lamar
Video Director of the Year
Benny Boom
Colin Tilley
Director X
Hype Williams
Kanye West
DJ of the Year
DJ Drama
DJ Envy
DJ Esco
DJ Khaled
DJ Mustard
Producer of the Year
DJ Mustard
Dr. Dre
Metro Boomin
Mike WiLL Made-It
Pharrell Williams
MVP of the Year
DJ Khaled
Drake
Future
Kanye West
Kendrick Lamar
Track of the Year
“All the Way Up” – Produced by Cool & Dre and Edsclusive (Fat Joe & Remy Ma feat. French Montana & Infared)
“Controlla” – Produced by Boi-1da (Drake)
“Hotline Bling” – Produced by Nineteen85 (Drake)
“I Got the Keys” – Produced by Southside (DJ Khaled feat. Jay Z & Future)
“Panda” – Produced by Menace (Desiigner)
Album of the Year
DJ Khaled – I Changed A Lot
Dr. Dre – Compton
Drake – Views
Fetty Wap – Fetty Wap
Future –DS2
Kanye West – The Life of Pablo
Best New Hip-Hop Artist
Anderson .Paak
Bryson Tiller
Chance the Rapper
Desiigner
Tory Lanez
Hustler of the Year
DJ Khaled
Drake
Future
Jay Z
Kanye West
Made-You-Look Award (Best Hip-Hop Style)
A$AP Rocky
Drake
Future
Kanye West
Nicki Minaj
Best Mixtape
Chance the Rapper – Coloring Book
French Montana – Wave Gods (Hosted By Max B)
Future – Purple Reign
Lil Uzi Vert – Lil Uzi Vert Vs. The World
Young Thug – Slime Season 3
Sweet 16: Best Featured Verse
2 Chainz – “No Problem” (Chance the Rapper feat. Lil Wayne & 2 Chainz)
Drake – “Work” (Rihanna feat. Drake)
Kendrick Lamar – “Freedom” (Beyoncé feat. Kendrick Lamar)
Kodak Black – “Lockjaw” (French Montana feat. Kodak Black)
Nicki Minaj – “Down in the DM” – Remix (Yo Gotti feat. Nicki Minaj)
Impact Track
J. Cole – “Love Yourz”
Jay Z – “Spiritual”
Jidenna – “Long Live the Chief”
Raury feat. Key – “Trap Tears”
Sir The Baptist feat. ChuchPeople – “Raise Hell”
People’s Champ Award
Desiigner – “Panda”
DJ Khaled feat. Drake – “For Free”
Fat Joe & Remy Ma feat. French Montana & Infared – “All the Way Up”
O.T. Genasis feat. Young Dolph – “Cut It”
Travis Scott – “Antidote”
Young Thug – “Best Friend”

VIDEO: Mpya Kid Ink Ft Jeremih & Spice ‘Nasty’

05:56:00
Hii video mpya ya rapa Kid Ink akiwa na rnb staa Jeremih na Spice, video inaitwa ‘Nasty’ kutoka kwenye mixtape yake ya Rocketshipshawty 2.

Picha: alikiba kuachia video kali mpya akiwa na warembo hawa wakali

10:12:00
Alikiba yuko mbioni kuachia silaha yake mpya. Staa huyo wa ‘Aje’ ameonjesha kidogo kile kitakachoonekana kwenye video ya ngoma yake mpya, na mashallah itakuwa na warembo haswaaa.Staa huyo ameshare picha akiwa mbele ya jumba la kifahari na warembo wanane jijini Johannesburg, Afrika Kusini alikokuwa huko mwezi uliopita.
Pia ameshare video akiwa na video queen aitwaye, Michaela Roy.

VIDEO: Mpya The Game Ft Jeremih ‘All Eyez’ Itazame hapa

09:56:00
Rapa The Game ametoa video ya wimbo wake mpya “All Eyez” ikiwa ni rekodi mpya baada ya kutoa wimbo wenye kiki la kulala na Kardashians “Sauce” weekend iliyopita. Kwenye hii kazi mpya ya ‘All Eyez’ The Game yupo na rnb staa Jeremih.

Wimbo wa “All Eyez” upo kwenye album mpya ya The Game iliyopewa jina “1992” na inategemewa kutoka Sept. 30.

Fiesta Mwanza kumdondosha Wizkid

07:25:00

Clouds FM wamethibitisha kumdondosha hitmaker huyo wa ‘Shabba’ Jumamosi, August 20.


“Kituuuuuuu #DealDone kwa mara ya kwanza ndani ya Mwanza #StarBoY wako @wizkidayo utatapata kumshuhudia LIVE juu ya jukwaa la #Fiesta2016 #Imooooo,” wameandika Clouds.
Hii itakuwa mara ya pili muimbaji huyo anakuja Tanzania. Mwezi October mwaka jana alitumbuiza kwenye viwanja vya Leaders Club jijini Dar es Salaam.

Hiki ndicho kiasi cha Pesa alichokuwa akilipwa Hanscana na Wanene Entertainment.

06:57:00
Kama ulikuwa una shauku ya kujua kiasi cha pesa ambacho muongozaji wa video nchini Hanscana alikuwa analipwa na studio za Wanene,uongozi wa studio hizo wametaja kiasi walichokuwa wakimlipa director Hanscana.
Akiongea kwenye kipindi cha funiko base,Gentriez ambaye ni mmoja watu wa ndani wa kampuni hiyo amesema Hascana alikuwa analipwa sjilingi milioni mbili kila mwezi na studio hizo na pia video zote alizokuwa akizifanya pesa zilikuwa zinaingia kwa Hanscana.
Wanene tulikuwa tunamlipa mshahara hata kabla kampuni haijafunguliwa tulikuwa tunamlipa na video alizokuwa akifanya pesa yote ilikuwa inaingia mfuko kwa Hascana kwa hiyo wanene walikuwa wamewekeza kwake lakini baada ya kufungua kampuni ilibidi kwenye kila kazi lazima kuwe na percent ya kampuni..tulikuwa tunamlipa milioni mbili kwa mwezi” alifunguka Gentriez

Rapa Young Thug abadilisha jina lake la kimuziki

06:52:00
Rapa mwenye mikogo tofauti kwenye muziki ,tabia na mavazi yake Young Thug amesema anampango wa kubadilisha jina lake na kujiita  ‘No, My Name Is Jeffery
Young Thug anategemewa kutangaza jina hili jipya muda wowote sasa kwa mujibu wa mmiliki wa lebo ya 300 ‘Lyor Cohen‘.
Jeffery imetajwa kuwa album mpya ya Young Thug yenye mastaa kama Elton John, Birdman, Swizz Beatz, na Floyd Mayweather.
Jeffery Lamar Williams ndio jina halisi la Young Thug na leo August 16 amefikisha miaka 25.

The Game ajitamba kuwa amelala na dada wote watatu wa Kim Kardashian.

06:46:00
Rapa The Game amejitamba kuwa amelala na dada watatu wa Kim Kardashian ila mpaka sasa hajawataja kwa majina. Kupitia wimbo wake mpya wa “Sauce,” The Game anasema amelala na Kardashians watatu .
Kwenye mtari huu The Game anasema “I used to f*** bhes that Usher Raymond passed off / Then I fed three Kardashians – hold that thought.
Kwenye wimbo huu “Sauce” into iliyotumika ni ya Dj Khaled na mwisho wa wimbo anasema “I got 99 problems, but the sauce ain’t one.” Game yupo studio akifanya album yake ya 1992,

VIDEO: Jah Prayzah ft Diamond Platnumz 'watora mari'

02:44:00

VIDEO:Mpya Nay Wamitego 'pale katipatamu' enjoy

12:23:00
baada ya onyo kali kutoka BASATA hatimaye Nay Wamitego afanikiwa kutoa video ya wimbo wake uliozua utata 'pale kati patamu'
 
Copyright © bakinamimi. Designed by OddThemes & VineThemes