Latest in Tech

NJIA 10 ZA KUJITIBU UCHOVU WA POMBE {HANGOVER}


hangover ni nini?
hii ni hali ya kujisikia vibaya inayowapata watu watu ambao wanakua wamekunywa pombe nyingi jana yake, dalili zake ni kuuma kichwa sana, kutapika, kuishiwa nguvu, kujisikia uvivu sana na kushindwa kufanya kazi.
hali hii huvumilika mara nyingi lakini wakati mwingine hali hua mbaya kiasi kwamba mtu huweza kulazwa hospitali kwa matibabu zaidi.
sasa wewe kama mywaji wa pombe ni vizuri ukazifahamu njia ambazo unaweza kuzitumia kutibu hangover kabla au baada kunywa pombe kama ifuatavyo.
kunywa maji mengi;maji ni matibabu makuu ya hangover kabla na baada ya kunywa pombe, kawaida pombe humfanya mtu akojoe sana na kupoteza maji mengi mwilini na hii ndio moja ya sababu kuu ya kupata hangover sasa kitaalamu ili kuzuia hangover unatakiwa unywe chupa moja ya pombe na glass moja ya maji kila wakati na ikitokea hukufanya hivo na umeamka asubuhi una hangover basi jitahidi unywa hata lita tatu mpaka nne siku hiyo.[angalizo;usinywe maji yote kwa pamoja, weka kwenye chupa unywe taratibu]

kula chakula chenye mafuta mengi kabla ya pombe; chakula kama nyama, samaki, kuku, sambusa na vingine hua na mafuta mengi...pombe ikikuta mafuta tumboni inapata tabu kufanya kazi haraka kuliko ikikuta tumbo halina kitu, hii huzuia hangover za kesho yake lakini ukishakunywa haikusaidii tena.
kunywa kahawa; kawaha kitaalamu inaitwa stimulant, hii ni nzuri kwako ambaye umeamka na hangover lakini una kazi za kufanya siku hiyo zinazohitaji umakini mkubwa hivyo kahawa itakuondolea uchovu na kukufanya uwe makini lakini kunywa na maji pia kwani kahawa hufanya mtu akojoe sana kama pombe.
meza dawa za maumivu; maumivu ya kichwa yakiwa makali kuna dawa unaruhusiwa kumeza kupunguza maumivu hayo mfano diclofenac, aspirin, ibuprofen...usinywe paracetamol au dawa yeyote yenye mchanganyiko wa paracetamol kwani ikiungana na pombe inaharibu maini
                                                             
fanya mazoezi; kama kichwa hakiumi sana fanya mazoezi yeyote kwani hii itakusaidia kupunguza pombe mwilini, na kukuletea mood ya kufanya vitu kwani ubongo hutengeneza homoni ya furaha yaani endorphine wakati wa mazoezi.
epuka kuzimua na pombe; huu msemo hutumika na walevi kwamba anaamka na pombe ili kuondoa pombe, hapana hii haifai kabisa kwani inaweza kukuletea ganzi mwilini na kukufanya uwe mtegemezi wa pombe kwenye maisha yako yaani bila kunywa pombe huwezi kufanya chochote.
                                                 
ongeza sukari mwilini;pombe hupunguza sana sukari mwilini na hii ni kwasababu maini
yanashindwa kutengeneza sukari ya ziada na kua bize kuondoa pombe mwilini hivyo unaweza kunywa juisi, soda au kula chakula. juice ni nzuri zaidi kwani hurudisha na madini yaliyopotea mwilini.
kunywa tangawizi na maji ya moto; chukua tangawizi isage kisha ichemshe na maji ya moto, hii itakuondolea kichechefu na kukuletea hamu ya kula.
rudi kulala; mara nyingi pombe huharibu mfumo wa usingizi hivyo mtu anaweza asipate usingizi wa kutosha kwa kushtuka ovyo usingizini, lala mpaka utakapoona usingizi umeisha ndio uanze shughuli zingine.
jiuepushe na mwanga mkali na sauti kubwa za kelele; mtu akiwa katika hali hii hawezi kuvumilia mwanga mkali na sauti kubwa hivyo kaa mbali navyo kupata nafuu.
                                                       

Share this:

Post a Comment

 
Copyright © bakinamimi. Designed by OddThemes & VineThemes